Sunday, June 14, 2015

Tuache ubabaishaji kwenye, tujenge soka hai




Na EMANUELI KAPINGA.

Mara nyingi tunachagua viongozi ambao hawawezi kuwajibika katika soka, mfano mzuri ni kutoka Simba sports kamati ya usjili ina mzaa na maendeleo ya klabu,Simba iliingia kwenye mgogoro na Ramadhani Singano maarufu kama “messi” hii ni wazi kuwa hatuna watu makini wakushughulika na mikataba ya wachezaji. Katika nchi zilizoendelea huboresha mikataba ya wachezaji mwaka au miezi sita kabla ya kuelekea ukingoni kama wanahisi mchezaji ana thamani kwao hii ni kwa ajili ya kupata faida zaida kwa timu zikatakomwitaji kwa kuwa mkataba uko wazi.

Simba wasisikitike wamwache Singano aondoke, hakuna namna kwamba alikuwa na thamani kwao au walihiitaji kufanya kupata faida kupitia yeye hivyo hakuwa na thaman kwao wamwache aende au waweke pesa mezani waache ubabaishaji.
Nimesikitika kusikia eti Azam Tv ndiyo chanzo cha kushuka kwa mapato kutokana na watu kutofika uwanjani, tuache visingizio ambavyo havina msingi na badala yake tuangalie tatizo liko wapi, kuna vituo maarufu dunian kama Sky Sports,  Super Sport zinarusha ligi bora ulaya na mapato katika klabu hizo ni mengi.

Adui wa yote ni sisi wenyewe tuangalie tatizo letu liko wapi. Aina ya mpira unaochezwa hauvutii watazamaji kwenda viwanjani na hivyo wachezaji hupendelea kujaa viwanjani dhidi ya mechi tatu kati ya Simba, Azam na Yanga. Katika vituo vya azam watazamaji wengi pia hushindwa kumaliza baadhi ya mechi nyingi kutokana na soka kukosa mvuto.
Juzi katika tuzo za soka Tanzania kumezua vituko, mimi binafsi siwelewi Shabani Kado amewezaje kuwa goli kipa bora uku akiwa ametemwa na timu yake ya Coastal Union, ni wapi duniani kipa bora amewahi kutemwa kwenye timu yake, na yeye Mbwana Makata amewezaje kuwa kocha bora mbele Pluijim na Juma Mwambusi wa mbeya city tujiulize adui yetu ni nani ili tuweze kuleta mabadiliko katika soka letu la Tanzania.

Binafsi naumia kuyaona haya hatukuzi bali tunaua soka, hebu tuache ujanja ujanja, tuwe wa wataalam tuhamasishe soka bora, tusijali pesa kuwaweka viongozi ambao hawaelewi maana ya usajili au kanuni za soka au vyanzo vya maendeleo katika timu eti kisa ni shabiki wa muda mrefu na analipia kadi ya uanachama.  

No comments:

Post a Comment